Friday, April 17, 2015

WAGENI WAENDELEA KUCHAPIKA AFRIKA YA KUSINI

Wageni wa endelea kupigwa Africa ya Kusini



Wageni waendelea kushambuliwa Africa Kusini

Raia wa kigeni ashambuliwa Afrika Kusini

Kumekuwa na mashambulizi zaidi usiku dhidi ya biashara zinazomilikiwa na raia wa kigeni nchini Afrika Kusini.
Polisi walitumia gesi ya kutoa machozi na risasi za mipira kutawanya umati kusini mwa mji wa Johannesburg ambapo gari na nyumba vilichomwa moto.

Msemaji wa polisi aliiambia BBC kuwa karibu raia mia mbili wa kigeni walikimbilia usalama kwenye kituo cha polisi lakini wakaondoka muda baadaye.

Usalama umedumishwa kufuatia mashambulizi yaliyowalenga raia wa kigeni ambapo watu watano wameuawa.
.
Rais Jacob Zua amelaani ghasia hizo na maandamano ya amani mjini Durban siku ya Alhamisi yalihudhuriwa na zaidi ya watu elfu kumi.
Mjulidhe na mwengine
By moffat gibson

No comments: